EAST AFRICA YOUTH TANZANIA

EAST AFRICA YOUTH TANZANIA

Wednesday, November 30, 2016

Rais Magufuli amuaga Rais Lungu wa Zambia


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amembatana na mgeni wake Rais wa Zambia, Mhe. Edgar Lungu wakiangalia ngoma ya asili wakati akimuaga baada ya kumaliza ziara yake ya siku tatu nchini, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.  Rais Lungu ameondoka nchini leo mchana kurejea nchini kwake.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Rais wa Zambia Mhe. Edward Lungu wakipeana mikono kwenye hafla ya kumuaga Rais huyo
Waheshimiwa Marais (waliosimama jukwaani) wakitoa heshima wakati wimbo wa Taifa ukipigwa katika hafla ya kumuaga Rais wa Zambia Mhe. Lungu iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Aziz Mlima na Rais wa Zambia Mhe. Edward Lungu wakipeana mikono kwenye hafla ya kumuaga Rais huyo

Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli akifafanua jambo kwa Rais wa Zambia Mhe. Edgar Lungu wakati akielekea kupanda ndege muda mfupi kabla ya kuondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,Jijini  Dar es Salaam.

Mhe. Rais Edgar Lungu akipungia mkono wananchi waliojitokeza uwanja wa Ndege kwenye hafla ya kumuaga

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zambia Mhe. Harry Kalaba wakiwa tayari kusoma tamko la pamoja la Waheshimiwa Marais kwa wanahabari (hawapo pichani) mara baada ya ziara.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisoma tamko la pamoja

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zambia Mhe. Harry Kalaba wakipeana mikono baada ya kuosoma tamko la pamoja (joint communique)

Rais Lungu atembelea Bandari ya Dar es Salaam na Kampuni ya Zamcargo

Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu akiangalia mfumo wa kielektroniki  (haupo pichani) wa kuharakisha ukaguzi wa mizigo katika bandari ya Dare es Salaam alipotembelea bandari hiyo. Rais Lungu aliwasili bandirini hapo mapema leo asubuhi akisindikizwa na Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga

Meza kuu ikifuatilia shughuli zilizokuwa zikiendelea wakati wa mapokezi mara baada ya kuwasili eneo la bandari ya Dar es Salaam


Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu akizungumza na wafanyakazi na wwadau mbalimbali waliojitokeza kumpokea alipowasili eneo la bandari ya Dar es Salaam

Rais wa Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu akionesha kwa hadhira zawadi ya mchoro wa eneo la bandari aliyokabidhiwa na Mkurugendi Mtendaji wa Bandari ya Dar es Salaam 

Picha ya pamoja

Rais wa Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu akiongea na wafanyakazi wa kampuni ya Zamcargo alipoitembelea kampuni hiyo mapema leo asubuhi

Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa na Rais wa Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu  wakiangalia namna ya utendaji wa mashine za kushusha na kupakia mizigo zinazo milikiwa na Kampuni hiyo (Zamcargo). Zambia Cargo and Logistics (Zamcargo) nikampuni ya serikali ya Zambia iliyopo nchini inayojihusisha na  usafirishaji, upakiaji na ushushaji mizigo katika bandari ya Dar es Salaam.
Moja ya mashine za kunyanyu mzigo ikiwa imebeba madini ya shaba

Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza walipotembelea kampuni ya Zamcargo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifafanua jambo kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Song Geum-Young wakati wa mazungumzo waliyoyafanya Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika masuala mbalimbali ya kudumisha uhusiano kati ya nchi hizi mbili (Tanzania na Korea) sambamba na kuzungumzia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini inayofadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Korea, ikiwemo  mradi wa Hospotali ya Muhimbili, Mloganzila na Mradi wa ujenzi wa Daraja jipya la Sarenda unatarijiwa kuanza hivi karibuni.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimsikiliza Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Song Geum-Young wakati wa mazungumzo 

Katika kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara Bi. Mindi Kasiga,wengine ni maafisa kutoka Wizarani wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea.          

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchi


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifafanua jambo kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Song Geum-Young wakati wa mazungumzo waliyoyafanya Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika masuala mbalimbali ya kudumisha uhusiano kati ya nchi hizi mbili (Tanzania na Korea) sambamba na kuzungumzia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini inayofadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Korea, ikiwemo  mradi wa Hospotali ya Muhimbili, Mloganzila na Mradi wa ujenzi wa Daraja jipya la Sarenda unatarijiwa kuanza hivi karibuni.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimsikiliza Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Song Geum-Young wakati wa mazungumzo 

Katika kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara Bi. Mindi Kasiga,wengine ni maafisa kutoka Wizarani wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea.          

Tuesday, November 22, 2016

Marekani na Jumuiya ya Afrika Mashariki Zatia Saini Makubaliano ya Ushirikiano wa $194 Milioni Kuimarisha Maendeleo ya Kikanda

Arusha, TANZANIA.
 Serikali ya Marekani na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wamezindua Makubaliano ya Msaada wa Malengo ya Maendeleo Kikanda (Regional Development Objectives Grant Agreement) katika makao makuu ya EAC huko Arusha, Tanzania. Kwa niaba ya Serikali ya Marekani, Shirika lake la Ushirikiano wa Kimataifa (USAID) litachangia kiasi cha $194 milioni kwa kipindi cha miaka mitano



Kiasi cha $30 milioni zitaisaidia moja kwa moja Sekretarieti ya EAC Secretariat, ilhali kitakachobaki kitagharamia wadau wengine wa kikanda katika juhudi zao za kuendeleza ajenda ya EAC ya utangamano kikanda.
Marekani na Jumuiya ya Afrika Mashariki Zatia Saini Makubaliano ya Ushirikiano wa $194 Milioni Kuimarisha Maendeleo ya Kikanda
Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania na EAC Virginia Blaser, Mkurugenzi wa USAID wa Kenya na Afrika Masharika Karen Freeman, na Katibu Mkuu wa EAC Balozi Liberát Mfumukeko walitia saini hati ya makubaliano.

Kaimu Balozi Blaser alitambua manufaa makubwa ya kukuza ushirikiano wa kikanda, akielezea kuwa Marekani inaunga mkono “serikali na mashirika ya kikanda kama EAC katika juhudi zao za pamoja kufungua fursa zilizopo za kikanda kwa manufaa ya watu wake,”

Mkurugenzi wa USAID Freeman alisisitiza mafanikio ya pamoja ya EAC na USAID katika miongo miwili iliyopita. “Kwa kurahisisha utaratibu wa forodha na mipaka, tumerahisisha kasi, gharama nafuu na biashara ya uhakika. Tumeongeza uwekezaji kwa kufanikisha mikataba ya kimataifa ambayo inakuza viwanda vya ndani na vya uzalishaji.”

Kwa makubaliano haya, jumuiya ya EAC na Marekani zitafanya kazi kwa pamoja kwa (i) kuendeleza utangamano wa kiuchumi kikanda, (ii) kukuza biashara na uwekezaji kati ya nchi wanachama na Marekani, (iii) kuboresha usimamizi endelevu wa maliasili katika Ziwa Victoria na mfumo wa ikolojia wa Mto Mara, (iv) kuboresha upatikanaji wa huduma ya afya ya pamoja maeneo ya mipakani na (iv) kuimarisha mpangilio wa uongozi wa EAC.
Kupata taarifa zaidi kuhusu taarifa hii, tafadhali wasiliana na Ubalozi wa Marekani Ofisi ya Habari simu: +255-22-229-4000 au baruapepe: DPO@state.gov.