EAST AFRICA YOUTH TANZANIA

EAST AFRICA YOUTH TANZANIA

Tuesday, December 13, 2016

Wizara ya Mambo ya Nje yakutana uongozi wa Taasisi ya Aga Khan kujadili masuala ya ushirikiano


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akitoa hotuba ya ufunguzi katika kikao cha wadau kilichoandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje kwa  ajili ya kujadili masuala ya ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Uongozi wa Taasisi ya Maendeleo ya Aga Khan "The Aga Khan Development Network" (AKDN). Kikao hicho kilifanyika tarehe 13 Disemba, 2016 katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa masuala ya Diplomasia katika Taasisi wa Maendeleo wa Aga Khan, Balozi Arif Lalani  akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya Taasisi hiyo iliyopo nchini. Balozi Lalani alieleza kuwa wataendelea kushirikiana na Tanzania katika kuhakikisha wanatoa huduma nzuri na zenye ubora hususan katika sekta za Elimu, Afya na masuala ya Utalii sambamba na kuangalia namna ya kuanzisha maeneo mengine zaidi ya uwekezaji.
Waziri Mahiga akifuatilia ya taarifa iliyokuwa ikiwasilishwa na Mratibu wa Mradi wa Chuo cha Aga Khan kinachotarajiwa kujengwa Jijini Arusha. Pembeni yake kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi na kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Sheria, Balozi Baraka Luvanda.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga (kulia) pamoja na Bi Lilian Kimaro, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia kikao.
Sehemu nyingine ya Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje  na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia kikao.
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation       Kikao cha wadau k ikiendelea.      

Thursday, December 8, 2016

Afrika ijifunze kutoka Korea

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Afrika ijifunze kutoka Korea, Mawaziri.
Nchi za Afrika zimehimizana kutumia sera , mbinu na mfumo wa maendeleo uliotumiwa na Jamhuri ya Korea kufanya mapinduzi makubwa ya uchumi, viwanda na teknolojia katika kipindi cha miongo michache iliyopita.
Hayo yamejiri kwenye Mkutano wa  Mawaziri wa  nchi za Afrika na Korea uliohitimishwa leo jijini Addis Ababa, Ethiopia.
"Katika miaka ya 1960 hali ya uchumi na mazingira ya Korea yalikuwa yanalingana na bara la Afrika, hivyo, mfumo ulioifanya Korea kufanya mapinduzi ya uchumi unafaa kutumiwa na bara la Afrika kwa kuwa mazingira yetu yanafanana".
Katika mkutano huo ambaoTanzania iliwakilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga, Mawaziri walielezea kuridhishwa na ushirikiano huo tokea ulipoanzishwa mwaka 2006, kwa kuwa unazingatia maslahi ya pande zote na haufungamani na masharti ya aina yoyote.
Walisema kuwa Bara la Afrika lina fursa lukuki zikiwemo maliasiri kama madini, mafuta na ardhi nzuri kwa kilimo.
 Rasilimali hizo miaka yote zimekuwa zikiuzwa nje bila kuendelezwa kutokana na ukosefu wa viwanda na teknolojia, hali iliyochangia  kwa kiasi kikubwa kulifanya bara hilo kubaki nyuma kimaendeleo.
Hivyo, kupitia jukwaa hilo la ushirikiano na Korea, bara la Afrika litapokea misaada ya fedha za maendeleo na teknolojia  itakayotumiwa kujenga viwanda vya kusindika rasilimali ili kuziongezea thamani.
Kwa kuwa maendeleo na amani na usalama ni vitu vinavyotegemeana, Mawaziri walisisitiza umuhimu wa kutunza amani barani Afrika kwa kushirikiana na Korea.
 Walibainisha masuala mbalimbali yanayotishia amani ya  dunia likiwemo tatizo la ugaidi wa kimataifa. Walikubaliana kuwa ugaidi ni changamoto ya ulimwengu mzima na ili ufumbuzi wake upatikane lazima wadau duniani kote washirikiane.
Ushirikiano wa nchi za Afrika na Korea unatimiza miaka 10 mwaka huu tokea ulipoanzishwa mwaka 2006. Kwa muktadha huo, ulisisitizwa umuhimu wa kufanya tathmini na ufuatiliaji wa miradi ya utekelezaji ili kubaini mafanikio mapungufu na changamoto.  Hiyo itasaidia kuchukua hatua stahiki katika kufikia malengo yaliyowekwa na umoja huo.
Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje wa Korea, Mhe. Yun Byung-se alieleza mafanikio ya ushirikiano huo tokea kunzishwa kwake. Alisema katika eneo la ushirikiano wa kiuchumi na Afrika, Korea ilikuwa mwenyeji wa Mkutano wa tano wa Mawaziri wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea na Afrika mwezi Oktoba 2016.
 Katika mkutano huo, Korea iliahidi kutoa Dola za Marekani bilioni 5 kwa ajili ya kusaidia masuala ya kiuchumi barani Afrika. Fedha hizo zinatarajiwa kuongezeka  mara dufu katika kipindi kijacho. Aidha, Korea inatarajia kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Jukwaa la ushirikiano wa viwanda kati ya Korea na Afrika katika wiki mbili zijazo.
Vile vile, Korea imeongeza mara dufu misaada ya maendeleo kwa bara la Afrika na ile misaada ya maendeleo inayohusisha nchi mbili (bilateral)  itaongezeka kutoka asilimia 24 hadi kufikia asilimia 35 itakapofika mwaka 2020.
Waheshimiwa Mawaziri walihitimisha mkutano wao kwa kuridhia nyaraka mbili ambazo ni Tamko la Addis Ababa na Mwongozo wa Ushirikiano kati ya Korea na Afrika. Mwongozo huo umeainisha miradi mbali mbali itakayotekelezwa katika kipindi cha miaka mitano 2017 - 2021. Maeneo hayo ni pamoja na: biashara, kuendeleza viwanda na uwekezaji; uzalishaji katika kilimo na kiwango cha mavuno; uchumi wa bahari, uendeshaji wa bandari na usafiri wa majini; kuwaendeleza vijana na kuwajengea uwezo wanawake.
Wajumbe walikubaliana kuwa mkutano ujao utafanyika Seoul, Korea mwaka 2021.
Imetolewa na: KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI, WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI.
TAREHE 08 DESEMBA 2016 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akisoma hotuba ya Tanzania kwenye Mkutano wa Nne wa Ushirikiano wa nchi za Afrika na Jamhuri ya Korea uliofanyika jijini Addis Ababa, Ethiopia tarehe 06 na 07 Desemba 2016.
Mhe. Waziri Mahiga akipitia makabrasha ya mkutano. Nyuma ya Mhe. Waziri ni Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na kwenye Umoja wa Afrika, Mhe. Naimi Aziz na Afisa wa Ubalozi huo, Bi Suma Mwakyusa.

Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje nao wakifuatilia mkutano huo. Kutoka kushoto ni Bw. Gerlad Mbwafu, Katibu wa Waziri, Bi. Berther Makilagi, Afisa Dawati la Korea na Bw. Benedict Msuya anayemwakilishsa Mkurugenzi wa Asia na Australasia.

Picha ya pamoja
 

Wednesday, November 30, 2016

Rais Magufuli amuaga Rais Lungu wa Zambia


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amembatana na mgeni wake Rais wa Zambia, Mhe. Edgar Lungu wakiangalia ngoma ya asili wakati akimuaga baada ya kumaliza ziara yake ya siku tatu nchini, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.  Rais Lungu ameondoka nchini leo mchana kurejea nchini kwake.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Rais wa Zambia Mhe. Edward Lungu wakipeana mikono kwenye hafla ya kumuaga Rais huyo
Waheshimiwa Marais (waliosimama jukwaani) wakitoa heshima wakati wimbo wa Taifa ukipigwa katika hafla ya kumuaga Rais wa Zambia Mhe. Lungu iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Aziz Mlima na Rais wa Zambia Mhe. Edward Lungu wakipeana mikono kwenye hafla ya kumuaga Rais huyo

Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli akifafanua jambo kwa Rais wa Zambia Mhe. Edgar Lungu wakati akielekea kupanda ndege muda mfupi kabla ya kuondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,Jijini  Dar es Salaam.

Mhe. Rais Edgar Lungu akipungia mkono wananchi waliojitokeza uwanja wa Ndege kwenye hafla ya kumuaga

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zambia Mhe. Harry Kalaba wakiwa tayari kusoma tamko la pamoja la Waheshimiwa Marais kwa wanahabari (hawapo pichani) mara baada ya ziara.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisoma tamko la pamoja

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zambia Mhe. Harry Kalaba wakipeana mikono baada ya kuosoma tamko la pamoja (joint communique)

Rais Lungu atembelea Bandari ya Dar es Salaam na Kampuni ya Zamcargo

Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu akiangalia mfumo wa kielektroniki  (haupo pichani) wa kuharakisha ukaguzi wa mizigo katika bandari ya Dare es Salaam alipotembelea bandari hiyo. Rais Lungu aliwasili bandirini hapo mapema leo asubuhi akisindikizwa na Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga

Meza kuu ikifuatilia shughuli zilizokuwa zikiendelea wakati wa mapokezi mara baada ya kuwasili eneo la bandari ya Dar es Salaam


Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu akizungumza na wafanyakazi na wwadau mbalimbali waliojitokeza kumpokea alipowasili eneo la bandari ya Dar es Salaam

Rais wa Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu akionesha kwa hadhira zawadi ya mchoro wa eneo la bandari aliyokabidhiwa na Mkurugendi Mtendaji wa Bandari ya Dar es Salaam 

Picha ya pamoja

Rais wa Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu akiongea na wafanyakazi wa kampuni ya Zamcargo alipoitembelea kampuni hiyo mapema leo asubuhi

Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa na Rais wa Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu  wakiangalia namna ya utendaji wa mashine za kushusha na kupakia mizigo zinazo milikiwa na Kampuni hiyo (Zamcargo). Zambia Cargo and Logistics (Zamcargo) nikampuni ya serikali ya Zambia iliyopo nchini inayojihusisha na  usafirishaji, upakiaji na ushushaji mizigo katika bandari ya Dar es Salaam.
Moja ya mashine za kunyanyu mzigo ikiwa imebeba madini ya shaba

Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza walipotembelea kampuni ya Zamcargo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifafanua jambo kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Song Geum-Young wakati wa mazungumzo waliyoyafanya Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika masuala mbalimbali ya kudumisha uhusiano kati ya nchi hizi mbili (Tanzania na Korea) sambamba na kuzungumzia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini inayofadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Korea, ikiwemo  mradi wa Hospotali ya Muhimbili, Mloganzila na Mradi wa ujenzi wa Daraja jipya la Sarenda unatarijiwa kuanza hivi karibuni.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimsikiliza Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Song Geum-Young wakati wa mazungumzo 

Katika kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara Bi. Mindi Kasiga,wengine ni maafisa kutoka Wizarani wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea.          

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchi


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifafanua jambo kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Song Geum-Young wakati wa mazungumzo waliyoyafanya Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika masuala mbalimbali ya kudumisha uhusiano kati ya nchi hizi mbili (Tanzania na Korea) sambamba na kuzungumzia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini inayofadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Korea, ikiwemo  mradi wa Hospotali ya Muhimbili, Mloganzila na Mradi wa ujenzi wa Daraja jipya la Sarenda unatarijiwa kuanza hivi karibuni.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimsikiliza Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Song Geum-Young wakati wa mazungumzo 

Katika kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara Bi. Mindi Kasiga,wengine ni maafisa kutoka Wizarani wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea.          

Tuesday, November 22, 2016

Marekani na Jumuiya ya Afrika Mashariki Zatia Saini Makubaliano ya Ushirikiano wa $194 Milioni Kuimarisha Maendeleo ya Kikanda

Arusha, TANZANIA.
 Serikali ya Marekani na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wamezindua Makubaliano ya Msaada wa Malengo ya Maendeleo Kikanda (Regional Development Objectives Grant Agreement) katika makao makuu ya EAC huko Arusha, Tanzania. Kwa niaba ya Serikali ya Marekani, Shirika lake la Ushirikiano wa Kimataifa (USAID) litachangia kiasi cha $194 milioni kwa kipindi cha miaka mitano



Kiasi cha $30 milioni zitaisaidia moja kwa moja Sekretarieti ya EAC Secretariat, ilhali kitakachobaki kitagharamia wadau wengine wa kikanda katika juhudi zao za kuendeleza ajenda ya EAC ya utangamano kikanda.
Marekani na Jumuiya ya Afrika Mashariki Zatia Saini Makubaliano ya Ushirikiano wa $194 Milioni Kuimarisha Maendeleo ya Kikanda
Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania na EAC Virginia Blaser, Mkurugenzi wa USAID wa Kenya na Afrika Masharika Karen Freeman, na Katibu Mkuu wa EAC Balozi Liberát Mfumukeko walitia saini hati ya makubaliano.

Kaimu Balozi Blaser alitambua manufaa makubwa ya kukuza ushirikiano wa kikanda, akielezea kuwa Marekani inaunga mkono “serikali na mashirika ya kikanda kama EAC katika juhudi zao za pamoja kufungua fursa zilizopo za kikanda kwa manufaa ya watu wake,”

Mkurugenzi wa USAID Freeman alisisitiza mafanikio ya pamoja ya EAC na USAID katika miongo miwili iliyopita. “Kwa kurahisisha utaratibu wa forodha na mipaka, tumerahisisha kasi, gharama nafuu na biashara ya uhakika. Tumeongeza uwekezaji kwa kufanikisha mikataba ya kimataifa ambayo inakuza viwanda vya ndani na vya uzalishaji.”

Kwa makubaliano haya, jumuiya ya EAC na Marekani zitafanya kazi kwa pamoja kwa (i) kuendeleza utangamano wa kiuchumi kikanda, (ii) kukuza biashara na uwekezaji kati ya nchi wanachama na Marekani, (iii) kuboresha usimamizi endelevu wa maliasili katika Ziwa Victoria na mfumo wa ikolojia wa Mto Mara, (iv) kuboresha upatikanaji wa huduma ya afya ya pamoja maeneo ya mipakani na (iv) kuimarisha mpangilio wa uongozi wa EAC.
Kupata taarifa zaidi kuhusu taarifa hii, tafadhali wasiliana na Ubalozi wa Marekani Ofisi ya Habari simu: +255-22-229-4000 au baruapepe: DPO@state.gov.


Wednesday, October 12, 2016

Tour in DRC Kongo with Ambassador A.Mahiga

THE Chair of the Southern African De-velopment Community (SADC)’s Organ of Politics, Defence and Security (Troi-ka) Ministerial Committee, Ambassador Augustine Mahiga, has started a three-day visit to the Democratic Republic of Congo (DRC) to assess the situation in the country.
His tour comes a few days after the Troika Chairperson, President John Ma-gufuli, pledged to dispatch foreign affairs ministers from three African countries to assess the political situation in the DRC.

Along with Dr Mahiga are Angolan Foreign Minister and Mozambique Dep-uty Defence Minister.

The mission seeks to meet different stakeholders, discuss the political situation and advise accordingly.

A statement released in Dar es Sa-laam yesterday by Ambassador Innocent Shiyo from the Department of Regional Cooperation in the Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation, said the protests organised by opposition parties that took place in DRC on Sep-tember 19 forced President John Magu-fuli to dispatch the mission.

“The volatile political situation, security and peace in DRC that was at-tributed to, partly, by protests that were organised by opposition parties and took place on September 19 to pressurise the National Electoral Committee (CENI) to announce the date for the General Elec-tion prompted the president to send the mission.It will meet different stakeholders in the country, evaluate the situation on ground and advise accordingly,” stated Ambassador Shiyo.

The mission was to take place be-tween October 4 and 5 but due to the visit by President Joseph Kabila to Tanzania it had to be rescheduled.

“After consultations between Presi-dent Magufuli and President Kabila dur-ing the tour, it was agreed the mission should take place from October 10 to 13.

In the delegation, there is the Execu-tive Secretary of SADC, Dr Stergomena Tax and senior officials from the Minis-try of Foreign Affairs and East African Cooperation, President’s Office and the Ministry for Defence and National Ser-vice,” Ambassador Shiyo said.

The 36th Ordinary SADC Summit of Heads of State and Government that was held from August 30 to 31 in Mbabane, Swaziland, elected President Magufuli to be the Chairperson of the Troika.

Angola is vice-chairperson and Mozambique is outgoing chairperson.

According to Ambassador Shiyo, the mission had met some people, including SADC member ambassadors in DRC; the Chief Mediator of the African Union; Mr Eden Kodjo, DRC Minister for For-eign Affairs; Chairperson of CENI; non-governmental organisations (NGOs) and religious institutionsAmbassador Shiyo said the mission was putting great emphasis on the need for dialogue as the only means to get out of the deadlock, necessity of political tol-erance and later to hold an election at a time to be agreed upon amicably.

The SADC meeting received re-port on efforts being taken by the DRC Government and some other political stakeholders to ensure the country moves peacefully during and after the general election.

Friday, July 1, 2016

Alama za Jumuiya ya Afrika Mashariki

Matumizi ya Alama za Jumuiya ya Afrika Mashariki

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inatoa wito kwa Taasisi za Serikali kuhakikisha kuwa zinatumia alama za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ambazo ni Bendera na Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Alama hizo zinatakiwa kutumika kwenye Ofisi za Serikali (Wizara, Idara zinazojitegemea,  mashirika ya umma na Wakala) sambamba na alama za Taifa yaani Bendera ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wimbo wa Taifa. 
Bendera ya Jumuiya inatakiwa kupepea sambamba na Bendera ya Taifa kwenye Ofisi za Serikali na Wimbo wa Jumuiya  nao unatakiwa kuimbwa sambamba  na Wimbo wa Taifa wakati wa shughuli rasmi za Kiserikali. 
Hatua hiyo ni utekelezaji wa Mkataba wa Uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambao katika kifungu cha 
7(a) umesisitiza Jumuiya hii kuwa ni Jumuiya ya watu, hivyo wananchi wa Tanzania watahusishwa katika hatua zote za Mtangamano. Aidha,  Serikali ya awamu ya tano 
(5) chini ya Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki itahakikisha kuwa Watanzania wanashirikishwa kikamilifu katika hatua mbalimbali za Jumuiya ili kuijua kwa madhumuni ya kunufaika na fursa mbalimbali zinazopatikana ndani ya Jumuiya hiyo.
Matumizi ya alama hizi ni njia mojawapo ya kujenga uzalendo na kumfanya Mwananchi ajisikie kuwa sehemu ya Ushirikiano huu. Aidha, Taasisi binafsi hasa Mashule na Vyuo wanasisitizwa kutumia alama hizi kama sehemu ya kuelimisha na kuhamasisha vijana kuhusu Jumuiya ya Afrika Mashariki
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki itaratibu zoezi la upatikanaji wa sampuli ya alama hizo kwa gharama za taasisi husika, hivyo Wizara, Taasisi na Ofisi za Serikali zinahimizwa kuwasiliana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa ajili ya ufafanuzi zaidi wa upatikanaji na matumizi ya alama hizo.

Mkurugenzi wa Masomo katika Chuo cha Diplomasia, Dkt. Watengere Kitojo naye akizungumza kuhusu Kozi zinazotolewa na chuo hicho ikiwemo Cheti, StaShahada, Shahada katika masuala ya Uhusiano wa Kimataifa
Au unaweza kutuma maelezo ya Press Card yako, picha ya ndogo (passport size) kwenye email ifuatayo; media@eachq.org, CC:oothieno@eachq.org.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 19 Mei 2016.

ITAMBUE JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI NA FURSA ZITOKANAZO NA UMOJA WA FORODHA WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI


Jumuiya ya Afrika Mashariki ni Taasisi ya Kiserikali

 

(inter-Governmental Organization), iliyoanzishwa

na nchi za Tanzania, Kenya na Uganda. Mkataba

ulianzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki ulisainiwa

tarehe 30 Novemba, 1999 na ulianza kutumika

rasmi mnamo tarehe 7 julai 2000. Nchi za Rwanda

na Burundi zilijiunga katika Jumuiya ya Afrika

Mashariki mwaka 2007.

Jumuiya ya awali ya Afrika ya Mashariki iliundwa

mwaka 1967 na kuvunjika mwaka 1977. Kuvunjika

kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977

kulitokana na sababu nyingi zikiwemo za kisiasa,

kijamii na kimaslahi. Sababu hizo ni pamoja na:

 

a. Itikadi tofauti za kisiasa zilizokuwa zikifuatwa

na Nchi Wanachama

 

b.Kutoelewana katika mgao wa mapato kutoka

katika Mashirika ya huduma za Pamoja na

kutokuwepo kwa Seraya kushughulikia tatizo

hilo;

c.Athari za vita baridi baina ya Amerika na

Urusi kwa wakati huo;

 

d.Ushiriki mdogo wa sekta binafsi na vyama

vya kiraia katika uendeshaji wa Jumuiya ;

na

e. Mtizamo finyu kuhusu mtangamano kwa

baadhi ya viongozi na watendaji.

Baada ya kuvunjika kwa Jumuiya, Nchi Wanachama

zilitiliana saini makubaliano ya kugawa mali na

madeni (mediation agreement for the divisionof assets

 

amhuri

 

ya

m

uungano

•Tanzania • B

MH. RICHARD KASESELA IRINGA DC KATIKA MAHAFARI YA EAST AFRICA CHUO KIKUU RUCU

Mkuu wa Wilaya ya Iringa DC Mhe Richard Kasesela

Leo alikuwa mgeni Rasmi katika mahafari  ya EASTAFRICA COMMUNITY EAC katika chuo kikuu RUCU

Ambapo ametoa  ushauri kwa wanafunzi kwa habari ya uwekezaji kipindi wakiwa shule mfano kwa Iringa kuna fursa ya upandaji Miti.

Kipindi anajibu RISALA Mhe. Mkuu wa Wilaya Richard Kasesela anasema kuandaa mpango kazi kwa lengo la kufanikisha malengo ya jumuiya ya UMOJA wa Africa Mashariki katika chuo cha RUCU. Pia ( fundarising proposal) 

kwa upande wa vyuo vikuu pia ametoa ushauri kuandaa mashindano ya vyuo vya hapa iringa mjini kwa lengo la kufanya Iringa kuwa kituo cha maarifa." Center of Knowledge "

Pia kwa upande wa Mchungaji ameongelea Misingi ya Maadili ni katika uchaji wa UPENDO, UMOJA,MSHIKAMANO NA AMANI 



 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

Jumuiya ya Afrika Mashariki

Jumuiya ya Afrika Mashariki au Mtangamano wa Afrika Mashariki (kwa Kiingereza East African Community, kifupi EAC)



Ni muundo wa kisiasa unaounganisha nchi tano za kanda ya Maziwa Makuu ya Afrika Mashariki: Burundi, Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda. Mnamo Machi 2016 Sudan Kusini imekuwa nchi wa sita.
Eneo la Mtangamano ni 1,820,664 square kilometres (702,962 sq mi), likiwa na wakazi 153,301,178 (kadirio la mwaka 2014)
Jumuiya yenye jina hilo imepatikana mara mbili katika historia: jumuia ya nchi tatu kubwa zaidi kati ya hizo ilianzishwa mwaka 1967, lakini ilisambaratika mwaka 1977
Jumuiya ilifufuliwa rasmi tarehe 7 Julai 2000.