EAST AFRICA YOUTH TANZANIA

EAST AFRICA YOUTH TANZANIA

Wednesday, November 30, 2016

Rais Magufuli amuaga Rais Lungu wa Zambia


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amembatana na mgeni wake Rais wa Zambia, Mhe. Edgar Lungu wakiangalia ngoma ya asili wakati akimuaga baada ya kumaliza ziara yake ya siku tatu nchini, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.  Rais Lungu ameondoka nchini leo mchana kurejea nchini kwake.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Rais wa Zambia Mhe. Edward Lungu wakipeana mikono kwenye hafla ya kumuaga Rais huyo
Waheshimiwa Marais (waliosimama jukwaani) wakitoa heshima wakati wimbo wa Taifa ukipigwa katika hafla ya kumuaga Rais wa Zambia Mhe. Lungu iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Aziz Mlima na Rais wa Zambia Mhe. Edward Lungu wakipeana mikono kwenye hafla ya kumuaga Rais huyo

Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli akifafanua jambo kwa Rais wa Zambia Mhe. Edgar Lungu wakati akielekea kupanda ndege muda mfupi kabla ya kuondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,Jijini  Dar es Salaam.

Mhe. Rais Edgar Lungu akipungia mkono wananchi waliojitokeza uwanja wa Ndege kwenye hafla ya kumuaga

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zambia Mhe. Harry Kalaba wakiwa tayari kusoma tamko la pamoja la Waheshimiwa Marais kwa wanahabari (hawapo pichani) mara baada ya ziara.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisoma tamko la pamoja

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zambia Mhe. Harry Kalaba wakipeana mikono baada ya kuosoma tamko la pamoja (joint communique)

Rais Lungu atembelea Bandari ya Dar es Salaam na Kampuni ya Zamcargo

Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu akiangalia mfumo wa kielektroniki  (haupo pichani) wa kuharakisha ukaguzi wa mizigo katika bandari ya Dare es Salaam alipotembelea bandari hiyo. Rais Lungu aliwasili bandirini hapo mapema leo asubuhi akisindikizwa na Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga

Meza kuu ikifuatilia shughuli zilizokuwa zikiendelea wakati wa mapokezi mara baada ya kuwasili eneo la bandari ya Dar es Salaam


Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu akizungumza na wafanyakazi na wwadau mbalimbali waliojitokeza kumpokea alipowasili eneo la bandari ya Dar es Salaam

Rais wa Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu akionesha kwa hadhira zawadi ya mchoro wa eneo la bandari aliyokabidhiwa na Mkurugendi Mtendaji wa Bandari ya Dar es Salaam 

Picha ya pamoja

Rais wa Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu akiongea na wafanyakazi wa kampuni ya Zamcargo alipoitembelea kampuni hiyo mapema leo asubuhi

Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa na Rais wa Zambia Mhe. Edgar Chagwe Lungu  wakiangalia namna ya utendaji wa mashine za kushusha na kupakia mizigo zinazo milikiwa na Kampuni hiyo (Zamcargo). Zambia Cargo and Logistics (Zamcargo) nikampuni ya serikali ya Zambia iliyopo nchini inayojihusisha na  usafirishaji, upakiaji na ushushaji mizigo katika bandari ya Dar es Salaam.
Moja ya mashine za kunyanyu mzigo ikiwa imebeba madini ya shaba

Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza walipotembelea kampuni ya Zamcargo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifafanua jambo kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Song Geum-Young wakati wa mazungumzo waliyoyafanya Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika masuala mbalimbali ya kudumisha uhusiano kati ya nchi hizi mbili (Tanzania na Korea) sambamba na kuzungumzia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini inayofadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Korea, ikiwemo  mradi wa Hospotali ya Muhimbili, Mloganzila na Mradi wa ujenzi wa Daraja jipya la Sarenda unatarijiwa kuanza hivi karibuni.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimsikiliza Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Song Geum-Young wakati wa mazungumzo 

Katika kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara Bi. Mindi Kasiga,wengine ni maafisa kutoka Wizarani wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea.          

No comments:

Post a Comment